KITENDA WILI"NYUMBA YANGU NDOGO LAKINI INAENEA WATU WENGI' MBUTA NANGA!!

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO BLOG

FLORA LYIMO BLOG

FLORA

FLORA

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA MH PINDA

FLORA NA MH PINDA

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

Saturday 23 April 2016

WHATS NOW ' STAY SEXY ITS FLORA LYIMO TZUK aka MBUTA NANGA! BIRTHDAY TODAY 'RUWA AIKA MBEE''

FLORA BAHATI  LYIMO aka MBUTA NANGA MTANZANIA ALISI AIPENDAE NCHI YAKE KUPITA MAELEZO '
Jamani leo ndiyo nilizaliwa pale Kilema Hospital Moshi Kilimanjaro Tanzania'' Kwa Familia ya Basilei Piusi Lyimo  Kama siyo Mama yangu Augustina Lyimo nisingejikuta hapa London Mji Mkuu wa Uingereza Leo '' Yani japo nipo kwa jihudi zangu na Maarifa yangu na Akili zangu aisee Bila Sala za Mama yangu na Sanam ya Mama Bikira Maria aliyo nipa pamoja na Rozari ili ziwe zinanilinda na kuniongoza kwenye njia njema 'Nisingekuwa nauwezo wa kumjengea Mama yangu hata kanyumba cha Bloku cha Room Moja ''badala yake nimeweza kuwajengea nyumba hata sijui zina Marum mangapi vile na room zingine wala hakuna watu maana wengi wetu tupo mamijini Hahahaah'' Jamani Furaha ya Mtoto Wa Kike ni Kuwajali Mama ,Baba Na Ndugu aliozaliwa nao kwanza maana ipo siku Utaolewa na Utasepa Nyumbani na Mijengo uliyojenga huko ikabakia tupu'' Anyway '' Nimejinyima mengi mno na nimeweza kufanya Mengi mno hasa nikiwafanyia Watu ,ndugu na Marafiki bila kujijali Mimi mwenyewe '  Ila yote hayo Nimeyaanza Mimi na kuyapoteza sina Wasi wasi kabisa maana najua kuyaanza '' RUWA MANGI 'I CANT SAY MUCH '' TODAY ITS MY BIRTHDAY ' THE #BOSSMBUTANANGA BIRTHDAY THE ONE AND ONLY IN THE WORLD''
ITS MAKE ME
feel Fabulous to be me #myself  and you my Jesus bila wewe now way I will ever FANYA NA KUJIVUNIA MAISHA YANGU '' I KNOW MYSELF AND I LOVE IT WHEN I CAN DO WHAT I WANT ''
MY JESUS I THANK YOU FOR MY ANGEL ,I THANK YOU FOR MY MAMA,MY BABA, MY NDUGU ZANGU ,MY FRIENDS (GOOD AND BAD ) WOTE HUWA NAJIFUNZA VITU FULANI FULANI KUTOKA KWAO, I THANK YOU FOR EVERYTHING ,I THANK YOU FOR ANYONE WHO COME IN TO MY LIFE (STAY AND GO) WOTE WAMENIACHIA VYA KUJIFUNZA NDANI YA MAISHA YANGU''
I THANK YOU FOR MY NUMBER ONE FRIEND MY JESSICA WHO WAS THE VERY FIRST MTANZANIA UK TO KNOW AND TO BEFRIEND WITH HER WAKATI NILIPOKUWA IN LONDON KUANZAIA 1995 IS WHEN URAFIKI WETU ULIPOZALIWA' SHE THEN GIVE ME A CUTE CLEAVER FABULOUS BABY BOY AJ'' I LOVE THEM SO MUCH '' THIS YER ALL I WANT FOR MY BIRTHDAY IS THEM''
I GIVE THEM MY LIFE FOR EVER '' LIKE THEY SAY ''UNAWEZA KUCHAGUA MARAFIKI LAKINI NDUGU HUWEZI KUWACHAGUA'
MY DEARS  I THANK YOU ALL AND BE BLESS ALWAYS'' JUENI NAWAPENDENI SANA SANA SANA''






 ITS FEEL FABULOUS '' JESUS I THANK YOU FOR MY FABULOUS LIFE''

 AND THATS WHAT WAS LEFT '' WAS YUMMY ''


 NAIPENDA NAIPENDA RANGI YANGU ASILI YA MWAAFRICA '' ISEE HAIPATIKANI POPOTE ULIMWENUNI ''HII UNAPEWA NA YESU PEKE YAKE'' IM SO BLESS''




FLORA LYIMO HOW TO LOOK SEXY AT HOME'' WHY IS THAT ? KWA SABABU I LOVE IT WHEN YOU ARE NDANI TO LOOK TOFAUTI NA WHEN YOU ARE OUTSIDE '' NDANI NI SEHEM PEKE YAKE AMBAPO UNAWEZA KUFANYA MENGI AMBAYO KWANZA KABISA ITS ONLY YOU AND ALOBAHATIKA KUKUWEPO NAWE NDANI HAPO CAN SEE KWANZA UYAFANYAYO AU UYATENDAYO THEN PUBLIC IF YOU WISH OR WANT '''
YOU SEE YANI HAPO UPO FREEE KABISA BILA HATA KULIPIA ANYTHING AU KUCHAJIWA ANYTHING '' JUST DO WHAT MAKE YOU HAPPY '' AND THATS IS ALL FLORA LYIMO aka MBUTA NANGA SHE IS ALL ABOUT ''
MAISHA KWANZA MAFUPI SANA '' NA BILA KUYATENDEA HAKI YANI UTAKUJA KUJUTAAAA' ISHI FOR TODAY '' ISHI FOR NOW'' MPO HAPO EEEE'' MAISHA NI YAKO MWENYEWE''
FLORA BAHATI LYIMO aka MBUTA NANGA!

Saturday 9 April 2016

WHATS NOW ? NI WAKATI WA KUSOMA SASA NA SIYO KILA SIKU KUTIZAMA TIZAMA PICHA TU'' NGACHOKA' TUMECHOTA NA KUMIMINA KUTOKA MATUKIO MICHUZI''

HOTUBA YA MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR, MHE. BALOZI SEIF ALI IDDI WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA TISA LA WAWAKILISHI, TAREHE 08 APRILI, 2016


1.  Mheshimiwa Spika, awali ya yote, sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu na Mwingi wa Rehma kwa kuendelea kuweka nchi yetu hii katika hali ya amani, utulivu, umoja na mshikamano mkubwa. Hali ambayo imeiwezesha Serikali na wananchi kuendelea na shughuli zao za kila siku bila ya mtafaruku wa aina yeyote. Aidha, tunaendelea kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kufanya uchaguzi katika hali ya amani na utulivu, jambo ambalo sote tuliomo humu Barazani pamoja na wananchi wote ni mashahidi wa hilo. Ninawaomba wananchi waendelee kuitunza na kuithamini amani iliopo nchini.

2.  Mheshimiwa Spika, kwa mara nyengine tena, napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutukutanisha hapa tukiwa katika hali ya uzima na afya njema na kutuwezesha kufanikisha vizuri Mkutano wa Kwanza wa Baraza hili Tukufu la Tisa la Wawakilishi, ulioanza tarehe 30 Machi, 2016. Nimefarijika kuwa kazi zote zilizopangwa katika ratiba yetu tumezikamilisha kwa wakati na kwa ufanisi mkubwa.

3.  Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kwa niaba yangu na Waheshimiwa Wawakilishi kutoa pongezi za dhati kwako wewe Mhe. Spika pamoja na Naibu Spika, Mhe. Mgeni Hassan Juma kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuliongoza Baraza letu hili Tukufu. Vile vile, nampongeza Mhe. Riziki Pembe Juma, Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Viti Maalum na Mhe. Shehe Hamad Mattar, Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Jimbo la Mgogoni, Pemba kwa kuchaguliwa kuwa Wenyeviti wa Baraza letu hili. Hii inaonesha imani kubwa waliyonayo Waheshimiwa Wajumbe juu yao. Ni mategemeo ya Waheshimiwa Wajumbe kwamba mtaliongoza Baraza hili Tukufu kwa hekima, busara, uadilifu na umakini mkubwa ili kuliwezesha Baraza kutekeleza majukumu yake yakiwemo ya kuisimamia Serikali kwa ufanisi na kupeleka maendeleo endelevu kwa wananchi wetu na nchi yetu kwa ujumla. 

Aidha, nachukua fursa hii kuwapongeza Waheshimiwa Hamza Hassan Juma, Salha Mohamed Mwinjuma, Rashid Ali Juma, Lulu Msham Abdulla na Hamad Abdulla Rashid kwa kuchaguliwa kwao kuwa Wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi.  Kuchaguliwa kwao kunadhihirisha imani kubwa ambayo Waheshimiwa Wajumbe aliyonayo juu yao, kwani Kamati hii ni muhimu sana kwa maendelezo ya Baraza letu.

Aidha, napenda kuwapongeza wenzetu saba walioteuliwa na Mheshimiwa Rais kuwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na hivi karibuni tu uliwaapisha.  Wajumbe hao wakiwa Mhe. Mohamed Aboud Mohamed, Mhe. Amina Salum Ali, Mhe. Maudline Castico, Mhe. Ali Abeid Karume, Mhe. Hamad Rashid, Mhe. Juma Ali Khatib na Mhe. Said Soud Said.  Kuteuliwa kwao kunaonyesha imani kubwa ambayo Mheshimiwa Rais anayo juu yao na kwamba michango yao italisaidia sana Baraza lako Tukufu.

4.  Mheshimiwa Spika, napenda kutoa pongezi maalum kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, kwa kuchaguliwa kwa ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 91 kushika wadhifa huo katika muhula wa pili wa Serikali ya Awamu ya Saba kupitia uchaguzi wa marejeo uliofanyika tarehe 20 Machi, 2016.  Aidha, pamoja na pongezi hizo, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Dkt.Ali Mohamed SheinRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa imani kubwa aliyoionesha kwangu kwa kuniteua kuwa Makamu wa Pili wa Rais kwa mara nyengine tena.  Namuomba Mwenyezi Mungu atubariki na kutujaalia afya njema na nguvu ya kuwatumikia wananchi wote hapa Zanzibar bila kujali rangi, jinsia, dini au itikadi zao za kisiasa.

5.  Mheshimiwa Spika, aidha, kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, napenda kutoa pongezi za dhati kwa Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi sana.  Hii imeonyesha imani na upendo kwa wananchi wa Tanzania walioayo juu yao.  Pia nampongeza Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuteuliwa kushika nafasi hiyo.  Hii inaonyesha imani ambayo Mhe. Rais Magufuli aliyonayo juu yake.

Ni matumaini yetu kwamba viongozi wetu hao watalitumikia Taifa letu kwa hekima na busara ili kuwapatia wananchi wetu maendeleo ya dhati.  Tunampongeza Rais Magufuli kwa kasi aliyoanza nayo.

6.  Mheshimiwa Spika, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein tarehe 05 Aprili, 2016 alilituhutubia Baraza hili Tukufu kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo Kikatiba. Pamoja na mambo mengine, katika hotuba yake amefafanua kwa kina kuhusu wajibu wetu kama Wajumbe wa Baraza hili, na ameeleza masuala muhimu katika kuijenga Zanzibar yetu.

7.  Mheshimiwa Spika, hotuba ya Mheshimiwa Rais itakuwa dira na mwongozo wetu katika kutekeleza majukumu yetu ndani na nje ya Baraza hili kwani hotuba hiyo iligusa kila Sekta ya maendeleo yetu.  Wajumbe mlipata nafasi ya kuijadili hotuba hiyo kuanzia tarehe 6 Aprili, 2016 hadi leo hii.

Michango ya Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza lako tukufu ilijikita zaidi juu ya uwepo wa amani na utulivu, kuboresha na kuimarisha maeneo huru hasa ya Fumba na Micheweni, vita dhidi ya rushwa na udhalilishaji wa kijinsia, wanawake na watoto, uendelezaji wa elimu na Vyuo vya Amali, mazingira, ajira kwa vijana, ukusanyaji wa mapato na ulipaji wa kodi kwa kutaja machache.  Naliahidi Baraza lako tukufu kuwa Serikali itachukua hatua ya kuyashughulikia mapendekezo yote yaliyotolewa.  Kama Mwanasheria Mkuu alivyosema, michango yote hiyo itawekwa kwenye jeduali maalum (Bango Kitita) na kusambazwa kwa Mawaziri wote watakaohusika.

8.  Mheshimiwa Spika, Baraza hili Tukufu la Wawakilishi lina jukumu muhimu na kubwa la kutunga Sheria. Napenda kuwakumbusha Waheshimiwa Wawakilishi kwamba hiyo itakuwa ndiyo kazi yetu ya msingi, inayotakiwa kufanywa kwa busara, hekima na umakini mkubwa.  Pia, tunalo jukumu la kuisimamia na kuishauri Serikali ili kuhakikisha kuwa matatizo na kero mbali mbali za wananchi zinatatuliwa kwa ufanisi na mafanikio makubwa.  Tunapaswa kuhakikisha kuwa Serikali inatoa mchango wake kikamilifu katika kuyafanya maisha ya wananchi wetu kuwa bora zaidi kwa kutumia nguvu kazi na rasilimali tulizonazo. Ni matarajio ya Serikali kuwa itapata taarifa na ushauri kutoka kwa Waheshimiwa Wawakilishi juu ya maeneo yanayohitaji kupewa msukumo ili kuongeza kasi ya maendeleo ya Zanzibar. Kwa upande wake, Serikali itaifanyia kazi taarifa na ushauri utakaotolewa na Baraza hili Tukufu.

9.  Mheshimiwa Spika, sambamba na majukumu hayo, naomba kuwashauri Waheshimiwa Wawakilishi tuwe karibu na wananchi waliotuchagua. Sisi ndio macho na masikio ya wananchi hao. Tumepewa heshima kubwa na wananchi hao kwa kutuchagua kuwa Wajumbe wa Baraza hili.  Wananchi hao wana mategemeo makubwa kwamba tutawasaidia kutatua changamoto zao mbali mbali za maendeleo zinazowakabili. Ni wajibu wetu kufikisha mawazo ya wananchi hao Serikalini kwa kupitia mikutano na vikao vya Baraza hili pamoja na njia nyengine zinazofaa. Aidha, tunapaswa kuwaeleza wananchi wetu kile ambacho Serikali imepanga kukifanya na jinsi ya kutumia fursa, rasilimali, mipango na taratibu zilizopo za Serikali ili kuweza kuboresha maisha yao.

10.    Mheshimiwa Spika, napenda kuwaomba kwa mara nyingine tena, wananchi wote kuendelea kudumisha amani na utulivu katika visiwa vyetu na nchi yetu ya Tanzania kwa ujumla. Bila ya kuwepo Amani na Utulivu, hakuna maendeleo. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kusimamia suala la amani na utulivu kwa nguvu zake zote ili kutekeleza mipango yetu ya kujiletea maendeleo zaidi ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.  Hakuna haja tena ya kukumbusha mambo yaliyopita, ila Serikali inatambua wapo baadhi ya wananchi wakorofi wanaojihusisha na vitendo vya kuvuruga amani na utulivu uliopo.

Kwa mfano, wakati tukielekea katika uchaguzi wa marejeo uliomalizika hivi karibuni, wakorofi hao walijihusisha kutega miripuko inayosadikiwa kuwa mabomu na kuchoma moto mashamba ya mikarafuu, nyumba na makaazi na maskani za CCM. Vyombo vya Dola vinaendelea na hatua za uchunguzi wa matukio hayo na baadae kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria.  Hakuna mtu atakayepona kuchukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa atabainika kutishia amani na utulivu tulionao.


11.    Mheshimiwa Spika, tunasikitishwa na mambo yanayotokea huko Pemba ambapo baadhi ya wafanya biashara kuwanyima wananchi wenzao huduma za kibiashara kama vile kuwauzia bidhaa au kuwapa huduma za usafiri kwa sababu za kiitikadi za kisiasa.  Jambo hili siyo zuri na ingefaa liachwe mara moja.  Serikali inalifuatilia kwa karibu sana suala hili na haitasita kumchukulia hatua mfanya biashara yoyote atakaye liendeleza jambo hili ikiwa ni pamoja na kumfutia leseni yake.

12.    Mheshimiwa Spika, kuhusu uchaguzi wa marejeo uliofanyika tarehe 20 Machi, 2016, nachukua fursa hii kuipongeza Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa kazi nzuri ya kusimamia na kufanikisha uchaguzi huo kwa mafanikio makubwa. Uchaguzi huo ulikuwa huru na haki, na ulipelekea ushindi mkubwa kwa Chama cha Mapinduzi kupitia kwa aliyekuwa mgombea wake, Dkt. Ali Mohamed Shein, ambaye kwa sasa anaendelea kuiongoza nchi yetu akiwa ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kipindi cha pili cha miaka mitano (2015 – 2020).

13.    Mheshimiwa Spika, kwa vile uchaguzi umekwisha, tunapaswa tuzidishe ushirikiano, mshikamano na umoja wetu katika kuijenga nchi yetu. Kwa upande wetu Waheshimiwa Wawakilishi turudi Majimboni mwetu ili tukashirikiane na wananchi kusukuma gurudumu hili la maendeleo.  Aidha, napenda kutumia fursa hii kuwaomba watumishi na watendaji wote wa Serikali watakaoteuliwa hapo baadae, kuwatumikia wananchi wote bila ya kujali itikadi zao za kisiasa. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inahimiza uwajibikaji zaidi na usimamizi mzuri wa fedha na rasilimali nyengine za umma katika ngazi zote.   Wafanyakazi kujituma na siyo kufanya kazi kwa mazoea jambo ambalo Rais wetu alilipigia kelele sana katika kipindi kizima cha kwanza.  Na hata hotuba yake aliyoitoa wakati akilizindua Baraza hili alisisitiza jambo hilo.  Nikimnukuu alisema:
“wapo baadhi ya watumishi wenye tabia ya kutoroka kazini, kuchelewa na hawazijali kanuni ziliopo za utumishi wa umma.  Wao hujifanya wababe mbele ya viongozi wao.  Wafanyakazi wenye sifa mbaya nilizozielezea katika kipindi hiki tutawachukulia hatua watakapobainika na kama hapana budi tutawafukuza kazini.  Hatuwezi kuwa na wafanyakazi waliokuwa hawana nidhamu.  Sasa basi, imetosha.
Waliopewa dhamana ya kuziongoza Idara mbali mbali za Serikali watapaswa watekeleze wajibu kwa kuwasimamia wafanyakazi walio chini yao.  Pindi kama hawatawawajibisha wafanyakazi wao, basi watawajibishwa wao.  Lengo letu liwe kutoa huduma kwa wananchi, kwani sote tunawajibika kwao; kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.”

14.    Mheshimiwa Spika, mimi najua ziko Idara na Mashirika ya Umma ambayo hayako vizuri kiutendaji na ambayo yanalalamikiwa sana na wananchi kwa sababu ya kutowajibika kwa watendaji wao.  Nawaomba Watendaji watakaoteuliwa pamoja na kazi zao za Maofisini, watenge muda kuzitembelea  Taasisi zilizo chini yao ili waone uwajibikaji wa viongozi wanaozisimamia Taasisi hizo.  Naahidi kumsaidia Mheshimiwa Rais katika kuyatumbua majipu yatakayojitokeza.  Nitamuomba Mhe. Rais aniunge mkono kwa uamuzi wowote nitakao uchukua dhidi ya mtendaji yeyote ambaye ataonekana hawajibiki vipasavyo, kwa sababu ya ama uvivu, uzembe, dharau au ubadhirifu.  Wako watendaji, Mhe. Spika, wanakatazia jambo la maendeleo kwa sababu ya ubinafsi. Watendaji hawa nao hatutawavumilia.

15.    Mheshimiwa Spika, naamini siyo baada ya muda mrefu Mheshimiwa Rais atateua Baraza lake la Mawaziri.  Ni imani yangu kwamba tutashirikiana pamoja na Watendaji watakao teuliwa ili kulisukuma gurudumu la maendeleo kwa manufaa ya wananchi wetu.  Natoa wito kwa watakaoteuliwa kuwa Mawaziri nao wasikae maofisini tu, wakipepewa na mafeni na viyoyozi, bali watenge siku waende vijijini wakaangalie wananchi wenye matatizo na waone namna gani wataweza kuwasaidia.  Kila Waziri kwa eneo linalomhusu.

16.    Mheshimiwa Spika, migogoro ya ardhi imekuwa changamoto kubwa kwa Serikali yetu katika kipindi kilichopita.  Migogoro mingi imekuwa ikisababishwa na baadhi yetu viongozi kwa sababu za kitamaa.  Kama hiyo haitoshi, baadhi ya wananchi wanaendesha ujenzi wa nyumba kiholela bila ya vibali vya kujengea na wakati mwingine katika maeneo yasiyo ruhusiwa kama vile kwenye maeneo ya vianzio vya maji na maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa miji ya kisasa.  Tunawatahadharisha waliojenga katika maeneo hayo.  Katika hotuba yake aliyoitoa wakati akilizindua Baraza hili, Mheshimiwa Rais alilizungumzia sana suala hili.  Niwakumbushe aliyosema, namnukuu:
“Napenda nitoe indhari kuwa Serikali haitomvumilia kiongozi wa ngazi yoyote ambae atajijengea tamaa na akajiingiza katika migogoro ya ardhi au akashindwa kutatua migogoro iliyopo katika dhamana yake.  Si siri kwani wapo baadhi ya viongozi waliojiingiza katika matatizo ya ardhi na kusababisha mzozo mkubwa kwenye jamii.  Migogoro ya ardhi ni kadhia ambayo tunataka tuimalize katika kipindi hiki cha miaka mitano ijayo.  Kwa hivyo, nawatahadharisha viongozi watakaopewa dhamana ya kushughulikia masuala ya ardhi wayazingatie maelezo yangu haya.”

17.    Mheshimiwa Spika, mnamo siku za hivi karibuni kumekuwepo na upandaji wa bei za bidhaa bila ya sababu za msingi.  Serikali inalifuatilia suala hili kwa karibu sana, na atakaye gundulika kupandisha bei kiholela atafungiwa leseni yake ya kuendeshea biashara mara moja.
18.    Mheshimiwa Spika, ninachukua nafasi hii kutoa wito maalum kwa Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza lako Tukufu kushirikiana na wananchi katika kuendeleza usafi wa mazingira na kutekeleza maelekezo yote ya Wataalamu wa afya ili kujikinga na maradhi ya miripuko kikiwemo Kipindupindu kwani ugonjwa huo bado upo, na namna moja ya kuuepuka ni kuweka mazingira yetu katika hali ya usafi.
Pia, ninaomba niwakumbushe Waheshimiwa Wawakilishi na wananchi tuzitumie vizuri mvua zinazoendelea nchini kwa kuendeleza shughuli za kilimo cha mazao ya chakula na biashara kwa lengo la kupata mavuno mengi zaidi na kujiongezea kipato. Sambamba na hayo, Serikali inaendelea kuwataka wananchi wanaoishi sehemu za mabondeni waendelee kuchukua hadhari wakati huu wa mvua zinazoendelea ili tuweze kuepuka athari na majanga yasiyo ya lazima.  Tunawasihi wananchi hao wahame kutoka mabondeni humo na kuhamia sehemu za juu ili kuepuka uharibifu wa mali zao na hata upotevu wa maisha yao.

19.    Mheshimiwa Spika, mwisho, ingawa si kwa umuhimu, napenda kumshukuru sana Spika wetu Mstaafu, Mhe. Pandu Ameir Kificho kwa kuliongoza Baraza hili kwa umahiri mkubwa kwa mudakwa miaka 20 mfululizo.  Mhe. Kificho aliliongoza Baraza hili kwa hekima, busara na uvumilivu mkubwa.  Ninamtakia kila la kheri na mafanikio mema katika shughuli zake za baadae. 
Lakini pia niwashukuru Mhe. Ali Abdulla Ali, Naibu Spika Mstaafu, Waheshimiwa Mgeni Hassan Juma na Mahmoud Mohamed Mussa ambao walikuwa Wenyeviti wa Baraza hili.  Ni dhahiri kuwa wote walituongoza vizuri katika kipindi chote cha miaka 5 iliyopita.  Nao nawatakia kila la kheri na mafanikio mema.

20.    Mheshimiwa Spika, napenda kuwashukuru wote waliotuwezesha kukamilisha shughuli zilizopangwa kwenye Mkutano huu wa Kwanza wa Baraza la Tisa la Wawakilishi kwa ufanisi mkubwa. Pongezi hizo zaidi ziwafikie watendaji wote wa Baraza hili la Wawakilishi wakiongozwa na Katibu, Dkt. Yahya Khamis Hamad.  Ni ukweli usiofichika kwamba tumeanza vizuri na ninaamini tutaendelea vizuri.  Mungu libariki Baraza hili, Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.  Lakini pia niwapongeze wakalimani wetu wa lugha ya alama ambao wamewawezesha Waheshimiwa Wawakilishi wenye ulemavu wa kusikia kufuatilia yote yaliyokuwa yakiendelea ndani ya Baraza.  Pia nawashukuru wanahabari kwa kufanya kazi ya kuwahabarisha wananchi wetu yale yaliyokuwa yakiendelea Barazani hapa.

21.    Mheshimiwa Spika, nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitawashukuru wananchi wangu wa Jimbo la Mahonda kwa imani kubwa walionipa kwa kunichagua kuwa Mwakilishi wao.  Nawaahidi kuwa nitawapa utumishi ulio bora na kutekeleza ahadi zote nilizozitoa wakati wa Kampeni.  Nawaomba wanipe ushirikiano wao ili tuweze kuendeleza Jimbo letu na kujiletea maendeleo.

22.    Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia niwatakie Waheshimiwa Wawakilishi kila la kheri na mafanikio mema katika kuwatumikia wananchi wao Majimboni mwao.  Aidha, nawatakia safari njema na ya salama ya kurudi Majimboni mwao, na hasa Wawakilishi wenzetu kutoka Pemba kwa sababu wao wana safari ndefu zaidi kuliko wenzao wa Unguja.

23.    Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, naomba sasa kutoa hoja kwamba Baraza lako Tukufu liahirishwe hadi siku ya Jumatano tarehe 18 Mei, 2016, saa 3.00 barabara za asubuhi.