Mahakama ya hakimu mkazi KISUTU jijini Dar es Salaam leo
imeahirisha kesi ya tuhuma za mauaji inayomkabili ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’ dhidi ya aliyekuwa mwana filamu
mahiri Marehemu STEVEN
KANUMBA.
Wakili wa Upande wa Serikali ELIZABETH KAGANDA akizungumza
mahakamani hapo amedai Upepelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kwamba kesi
hiyo itatajwa tena 07/05/2012"
Umati mkubwa ulijitokeza katika mahakama hiyo kwa lengo
la kufuatilia mwenendo mzima wa kesi hiyo ambayo imevuta hisia za watu wengi
hapa nchini.
Hii ni
mara ya Pili kwa ELIZABETH MICHAEL kupandishwa Kizimbani kosa la mauaji ya mwana filamu huyo mnamo
April 7 2012 eneo la Sinza
Vatican Jijini Dar es Salaam.
ASANTE CARTHBERT
ANGELO KWA PICHA HIZI"
MISS FB FLORA BAHATI LYIMO SAY:
Mimi kwa kusema kweli sioni ni kwanini kumpandisha kizimbani leo kwa mara ya pili na bila kusema chochote au kuairisha ,je walesema ni kwanini kuairisha ,na je anaweza kuwekewa mzamana au ? na ikiwa hawajapata maelezo kamili yanayoyahitaji ni kwanini kumshikilia ? yani mimi namuonea huruma sana huyu dogo wetu kwani inawezekana kuna mengine ndani ya kusababisha kifo hichi cha Marehemu Steven Kanumba na hakijulikani.JE huyo Lulu wamesha mruhusu kuongea ? na amesemaje ?"
Pengine jamii nayo ingeungana kutaka kujua nini hasa kinaendelea kama vipi wamuachie mtoto wa watu mpaka pale watakapojua nini hasa kilichomsababishia kifo chake"Mara tu wakati madactari watakapotoa ripoti yao ndo hapo ukweli utakapojulikana zaid.so MIMI NINGEOMBA WAMUACHIE KAMA HAWAJAPATA USHAIDI KAMILI"
No comments:
Post a Comment