KITENDA WILI"NYUMBA YANGU NDOGO LAKINI INAENEA WATU WENGI' MBUTA NANGA!!

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO BLOG

FLORA LYIMO BLOG

FLORA

FLORA

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA MH PINDA

FLORA NA MH PINDA

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

Monday 26 May 2014

BY FLORA LYIMO ~ NIWIENI RADHI KWA PICHA HIZI '' POLICE PAMOJA NA MAJAMBAZI WAULIWA KINYAMA IN DAR'' HAWA NI NDUGU ZA WATU JAMANI YASIKITISHA MNO'''



 Mwili wa askari aliyeuawa ukiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Temeke
Askari polisi mmoja wa kituo cha polisi Chang'ombe, Mkoa wa kipolisi wa Temeke, ameuawa kikatili siku ya ijumaa mchana baada ya kupigwa risasi ya kifua na majambazi waliokuwa wanajaribu kutoroka baada ya kufanya tukio la kihalifu. Askari hao waliokuwa doria katika eneo la Wailes walijikuta wakishambuliwa kwa risasi na majambazi hao mara baada ya majambazi hao kujaribu kukimbia katika eneo la tukio kwa kutumia usafiri wa pikipiki kipindi ambapo askari polisi walikuwa karibu na eneo la tukio. Hata hivyo wakati askari hao wakijaribu kuwafukuza majambazi hao wawili kwa lengo la kuwakamata ndipo jambazi mmoja alitoa bastola na kumpiga risasi ya kifua askari huyo na kufariki pale pale.


Mwili wa askari huyo ukiwa umehifadhiwa.
Hata hivyo katika harakati za kujaribu kukimbia majambazi hao walianguka na pikipiki waliyokuwa wakitumia ndipo wakaamua kutimua mbio mitaani na kuingia katika nyumba moja ambapo walijificha na kujifanya kama ni wakazi wa eneo hilo, baada ya wnanchi na polisi kufika katika nyumba hiyo, baadhi ya majirani waliwaambia polisi kwamba wameona watu hao wameingia katika nyumba hiyo. Baada ya polisi kuingia waliwakuta watu hao wakiwa wametulia kama kwamba wao ni wakaazi wa nyumba hiyo na wala hawajui lililotokea.


Mwili wa mmoja wa majambazi ukiwa chumba cha kuhifadhia maiti 

Baada ya kuwatambua watu hao, polisi waliwatia nguvuni huku wananchi wenye ghadhabu waking'ang'ania kuwa wanataka kuwaua sababu wameshaua askari mmoja. Baada ya vuta nikuvute kati ya wananchi na askari hao ambao walikuwa wachache, wananchi walifanikiwa kuwachukua majambazi hao kwa nguvu kutoka mikononi mwa polisi na kuanza kuwapiga kwa silaha mbalimbali za kienyeji yakiwemo mawe na marungu mpaka watuhumiwa hao wakapoteza maisha.



Mwili wa jambazi mwingine ukiwa umeharibika vibaya baada ya kipigo kikali kutoka kwa wananchi wenye hasira.



Mwili wa askari polisi ukiwa umepakiwa kwenye gari ya polisi tayari kupelekwa hospitali ya Temeke kuhifadhiwa.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo waliiambia blogu hii kwamba majambazi hayo kabla ya kupambana na polisi walikuwa wamefanya uvamizi na kumuibia mwanamke mmoja mkazi wa eneo hilo. Hata hivyo mali au fedha iliyoibiwa haikuweza kujulikana mara moja.
THANKS KWA MRUSHA PICHA HIZI  NA HABARI 
Follow:FLORA LYIMO FASHION POLICE BLOG

No comments:

Post a Comment