Ule msemo wa ukisema cha nini wenzako wakiona cha maana na mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi umedhihirika pale ambapo kijana mzoea ma sugar mammy amejikuta akiangukia kwenye suga mammiest zaidi ya aliyekuwa nae awali.

Inasemekana Ezden the roker yule mtalaka wa dida shaibu ameingia katika penzi jipya na Flora Lymo a.k.a MBUTA NANGA ambae amekufa na kuoza kwa kijana Ezden. Habari kutoka kwa watu wa karibu na wahusika hawa zinasema tayari ticket imekatwa tayari kwa Ezden kukanyaga viunga vya jiji la London ili kumsalimia mpenzi wake mpya Flora Lymo. Kwa faida ya wengi ni kwamba Flora ndiye aliyetupa nyavu kwa Ezden na kijana bila hiyana akanasa nyavuni. Kama mambo yataenda sawa kijana Ezden anaweza kuhamia nchini Uingereza na kupata uraia wa huko kwani bibie tayari ana kibali cha kudumu cha makazi ya nchi hiyo kama sio uraia kabisa.

Kwa habari hizi yule mtoto wa king majuto alaiyekuwa ametuma maombi kwa florah lymo asahau tu kwani kete imemwangukia Ezden the rocker.

Hahaha ila Ezden kwa kuparamia mamama hahaha hujambo. ujue florah ni 40yrs anaitafuta 41 heri hata dida ni 30's.

Nawatakia kila la heri katika mapenzi yao...kumbuka mapenzi si sura, umbo wala umri. Dida mchuma ndio unaondoka huoooo kitu U.K.