KITENDA WILI"NYUMBA YANGU NDOGO LAKINI INAENEA WATU WENGI' MBUTA NANGA!!

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO BLOG

FLORA LYIMO BLOG

FLORA

FLORA

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA MH PINDA

FLORA NA MH PINDA

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

Sunday 20 January 2013

PICHA ZIMEONGEZWA HAPA NA PIA SOMA YALONIPATA NIKIWA AIRPOT "(ALBUM ONE) DIARY YA FLORA LYIMO FASHION POLICE HOME HOLIDAY IN TANZANIA 2012/13. IN ROMBO WITH RADIO MARIA "

















 My FAB big Sis katikati yani hapa ndo mara ya kwanza atiana machoni na Mdogo wake Flora Lyimo Fashion Police kwa muda wa miaka minne" was Shagwee but you know hapa ndo wanaingia kanisani na hatungeweza kukumbatiana wala kucheka sanaaaa you can see kicheko chake hapo ,yani I was so so Happy kumuona and si wezi kumshukuru Mungu na Mama Maria kwa Baraka zao zaidi " kwani hata sala zimeniishia nawaomba sana yani Sala ni Muhim sana my dears,HASA ROZARI!!

 Mmoja wa masista MABIBI ambao walikuwa nao wanasherekea miaka hamsini ya utawa" Bless them na zidini kutuombea tafadhali masista wetu"

 Hapa ni mpango mzima wakuingia kanisani yani palikuwa hapatoshi kabisaa!!

 Kanisani kulijaa kinoma kwa wale walokuja kuchelewa walikuwa hawana hata nafasi yakusimama ndani licha ya kukaa!

 Mtu na mtoto wa Dada yake, yani utadhani ni Mdogo wake !! 
 Mtu na mdogo wake ,hawa ni watoto wa Kaka yangu Mdogo na wa mwisho kwenye familia yetu"sasa hako kadogo kakuchoto Sista aliyetuleta hapa ambae ndo Dada yangu Mkubwa anampenda mno,you know nilipokuwa London nawanunulia nguo nyeupe kama nilivyoajizwa na wahusika Huyu mtoto mdogo hakuwepo kwenye Hesabu ,ila kufika Sista akauliza kina nani na nani watoto wadogo wanakuja,si akahesabiwa na huyu hakuwepo,yani akasema ni lazima akuwepo kama haji na wengine wasije,,,Mbuta Nanga,Sista wetu ni mkali nyie acheni tu,so what I did ,is Nililazimika kwenda kununua nguo nyingine pale Moshi mjini na kukamilisha sare ya watoto wengine wa wili ili zile nguo za Ulaya nilizopeleka zivaliwe na huyu ambae Sista kamzimikia,yani just to make her day you know siyo Siku kuu yetu ni yake na navyompenda lazima nihakikishe she is happy "thats is what I do hapa Duniani to make people Happy Hasa Ndugu zangu ,kwani unaweza kuchagua kila kitu lakini Ndugu zako ukishazaliwa nao huwezi kuwachagua kamwe"na vile vile ndo Umuhim wangu na sababu yakuishi na Furaha daima" FLFP.Ishi maisha yako and love God zaidi"
 Hapa Masista ndo walianza kutoka kanisani na kufuatiliwa na Wengine wote"




 Wazee wakutana Bless them kwa kweli " 

 Here she is,,Sista wa Lyimo ndo huyoo,,cheka sasa Sista wetu jamani unaruhusiwaa" yani huwa hachekaji chekaji ovyo " We love you so much Dada letu kubwa la kumtumikia Mungu na Mama Maria wa Kilimanjaro" Tuombee Daima Dada "

 Kicheko ndo hichooo,,acha weee,yani hapa nilipokuwa nampiga picha hii nlikuwa na jaribu sana kumchekesha hadi nikajichokea ila nikapata hicho kidogo ,Ruwa Mangi!

 In Love with hii picha jamani is the Best of zote I think " au nyie mwaonaje Nyota za FLFP"
 Tabasam nipate Furaha,siunajua nakupenda Dada,Tabasam wewe ndo Nyota yetu ,siwajua tunavyokupenda Dada Lyimo"




 I love with hii pia jamani hebu waangalieni miguuni NYeupee,hakuna alochafua chezea wao "The Flora Lyimo Fashion Police :say ..hivi ndivyo shereheni kunavyotakikana kama ni nyeupe ni nyeupe tu" akijamchafuaji anabakia nnje ya mpango mzima"








 Hapa wakiwa kanisani wakisikiza Misa yao kwa Makini"Dada yetu Mkubwa ndo huyo SISTA MARIA CARITAS watatu kulia" Zidi kutuombeeni sie wakosefu Masista wetu " We love nyie sanaa"

 Hawa ndo waliokuwa wanaongoza kwa Mauno kanisani jamani walicheza mpaka basi ,kweli niliamini Kuwa Sista siyo kwamba kunakuzuia kufanya Mambo yote,mengine kama kukata mauno unaruhusiwaa" yani subirini Video yao yaja soon"

 Hawa waliamua kuvaa hivi kama Dress Code yao kwani hata wao wana Sista wao ambae alikuwa anasherekea miaka yake Hamsini " na sisi our Dress Code was Blue and white"
 Radio Maria ndo hao wanawakilishaje,I love you Radio Maria na asanteni kwa kazi zenu njema hasa kukuwepo nasi siku hii muhimu ya Masista wetu "

So I went Here Fasta Fasta " Hapa pahali pakuombea unakwenda kumuomba Mama Bikira Maria kitu chako fasta fasta na kuingia kanisani,yani Lazima utakipewa kwani hapa hapasaliwi ovyo ovyo na wala kuingia asiye na mapenzi mema na binadam, na hata kama kuna mtu anakutendea au keshakutendea maurogi rogi yake au chochote ,,kitamrudia mwenyewe" kwani UNAVYOTAKA KUMTENDEA  MWANA WA MWEZIO MABAYA.NA WAKWAKO AU WEWE MWENYEWE AKITENDEWA UTAJISIKIAJE?, Hapa ndo maana unaambiwa ni pakuomba tu ,,Chumvi kwenye chakula ukiitia humo si lazima unaonjo kama imekolea ee,,na Hapa penye maombi Utaionjo chumvi uloitia kwenye Chakula upende usipende""Yani kama umemtendea mtu mabaya yatakurudiaje fasta" Bikira Maria Mama wetu wa Kilimanjaro na wa Mbinguni uzidi kutuombea na kutuonyesha maadui wetu hasa kuwaangamiza Amen"



 Magari ya Nguvu yalihuu""yani kukodisha Gari kutoka Moshi mjini kwa my Hotel kuanzia asubuhi saa mbili mpaka Jioni saa kumi na mbili ,kuturudisha Moshi Mjini" nilimlipa TZ shilingi Laki mbili ,ambazo ni kama £100. yani hapa Ulaya utakodisha gari gani kwa hela hizo" hata Limo unalipia £20 kwa mtu mmoja licha ya masaa yote hayo " so jamani Tanzania ukiwa na hela ni Raha na wanakuona kama Malikia wa Ulaya.I cant wait kurudi "


Flora Lyimo Fashion Police akanyaga Rombo Huruma kwa masista kutoka Ulaya,Mungu ni mwema sana na kwa kweli Shetani narudia tena Ashindwe na alishindwaje,maana Nilianza kuamini  Kuna mavisirani nimewekewa si mchezo wakati nilipokuwa Heatrow Airport London niliachwa na Ndege,why huwezi kuamini eti naanguka mbele za wanaokagua mizigo yani pale check in mizigo ,nikaangukia sanduku na mkono ukawa unauma ila nikajifanya nikama hauumi na kutaka kuendelea kucheck in,lakini wakanikatalia na kuniambia wewe umeumia huwezi kuingia kwenye hii ndege mpaka tukuitie Daktari atuambie kwamba upo powa ,I was like ok ,but si ndege itaondoka au mtanisubiria,hapana madam ,ndege itaondoka wewe nifuate utabidi uondoke na ndege nyingine,what >>?? yani bado nilikuwa in shock " so nani atalipa hiyo ticket ? ni wewe madam hilo siyo kosa letu nikosa lako mwenyewe,Uwii jamani hapa pamekuwaje Kosa langu mweneywe ? yani machozi yalianza kunitoka taratibuuu,,ok madaam hata ukilia haisaidi kitu wewe omba mungu hujaumia alafu utaenda kesho " then,Dactari wakaja na Ndege ishaniacha na mkono haujavunjika wala kuteguka,Na nikakataa kwenda Hosp kuufanyia uchunguzi ,yani Kudadadeki niliamini hapa si bure ,nikaanza kusali nikaenda kuchukua kahoteli hapo hapo nikalala na kuanza kufikiria safari ya kesho asubuhi nikaamka na kukata ticket nyingine hapo hapo nikajikuta next day nipo angani na kutua Africa salama" Eee Binadam jueni kwamba Watu wengine si wakuchezea ni Watu wa Mungu na wanaomba Mungu kupita maelezo ,nami ni mmoja wao " Naomba Mungu sana na Najua huwa ananisikiliza sala zangu kwani Hii safari nilienda kwasababu Mungu ndie aliyetaka niende na Siyo kiumbe chochcote" Bwana asifiwe sana" na Tumsifu Bikira Maria sana" Salini sana Rozari na Mzibebe kwenyewe Mabegi yenu Kina Mama/Dada ,tunaambiwa huo ndio ufunguo wetu wakuingia Mbinguni"(Rozari)yani ifanye leo kuwa kitu chako cha muhim kulikoni" FLFP.Whatsapp +44 7787471024"
Posted by Picasa

3 comments:

  1. Nice photos na hongera sana flora inaonekana una wapenda sana ndugu zako jamani na kumbe hata mna mpaka sista.Bless nyie sana mangi"

    ReplyDelete
  2. ahahaahhahaha...safi sana Flora...unajua haswaa kuweka utamu kwenye story..Kumbe mna sista kwenye familia?Haya mbarikiwe...umenichekesha sana kusema mauno yanaruhusiwa kwa masista...ahahhahahahha...hujatulia kiukweli..

    ReplyDelete
  3. Da'Flora Lyimo nimependa picha na Familia yako sana sana mzidi kubarikiwa na kutuombea maana kwenye familia kushakuwa na sista au padri ni Baraka tosha kutoka kwa Mungu'' hivi hapo ndo kijijini kwako flora''

    ReplyDelete