KITENDA WILI"NYUMBA YANGU NDOGO LAKINI INAENEA WATU WENGI' MBUTA NANGA!!

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO BLOG

FLORA LYIMO BLOG

FLORA

FLORA

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA MH PINDA

FLORA NA MH PINDA

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

Saturday 20 July 2013

BY FLORA LYIMO~ HABARI ZA UBAKAJI' (RAPE)SISTA WA KANISA KATOLIKI ABAKWA NA KUNDI LA WANAUME WA TATU' DUNIA INA ELEKEA WAPI ? MUNGU WANGU''

 


Sista aliye mafunzoni ametekwa na kubakwa kwa wiki nzima na kundi la wanaume watatu katika kile kinachohisiwa kuwa ni shambulio la kulipiza kisasi, vyombo vya habari nchini India vimeripoti.

Sista huyo mwenye miaka 22 alidaiwa kutekwa kwenye stesheni ya treni na binamu zake na kisha kushikiliwa mateka na kubakwa kwa zaidi ya siku kadhaa sababu waliishutumu familia yake kwa kifo cha baba yao.
 

Ni tukio la karibu kabisa katika mfululizo wa mashambulio ya ubakaji nchini India mwaka huu tangu mwanafunzi alipobakwa na kundi la wanaume na kufa kutokana na majeraha yake ya kutisha ndani ya basi la Delhi Desemba mwaka jana.
 

Sista huyo aliwaeleza polisi alikuwa akutane na binamu zake kwenye stesheni ya treni karibu na Chennai, huko Tamil Nadu, kusini mwa India, baada ya kudai kwamba mama yao alikuwa anaumwa.
 

Hatahivyo, anasema alichukuliwa hadi kijiji cha jirani ambako alishambuliwa mara kadhaa.
 

Watuhumiwa hao baadaye walimrejesha kwenye stesheni hiyo na kumwonya asiripoti tukio hilo.
 

Binamu wa mwanamke huyo, Jotindra Sobhasundar mwenye miaka 30, na Tukuna Sobhasundar mwenye miaka 28, walikamatwa Jumapili, kwa mujibu wa ripoti.
 

Mtuhumiwa wa tatu alikamatwa Jumatatu baada ya mfululizo wa makimbizano katika wilaya ya Kandhamal.
Vyombo vya habari za mjini humo vilisema kaka wa Sista huyo alihojiwa kuhusiana na mauaji ya mmoja wa watuhumiwa. 

 
Shambulio hilo lilidaiwa kutokea kati ya Julai 5 na 11 lakini likatangazwa hadharani wiki hii.

Tukio hilo limelaaniwa vikali na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki nchini India.

Kardinali Oswald Gracias, alinukuliwa akisema: "Ubakaji huu wa makundi ni ugaidi wa kimwili na kihisia.

Pia alizishutumu wakala za serikali kwa 'kukwepa wajibu wao'

Flora Lyimo~HABARI KAMA NILIVYOIKUTA KWENYE  BLOGS ZINGINE''

No comments:

Post a Comment