- Mimi nikiwa Mwana CCM na Kiongozi pia wa CCM ngazi ya Taifa na Blogger, naomba kusimama mbele ya Mheshimiwa Mbunge Kapuya na Taifa zima la Tanzania pamoja na wasomaji wangu wote wa Blog na meble ya Mungu, kukubali makosa na kuomba radhi, kwake na kwa Mungu wangu zaidi. Mimi ni mmoja wa watu wa kwanza kuamini hadithi iliyojitokeza hivi karibuni kwamba Mheshimiwa Kapuya amembaka na kumuambukiza Ukimwi na kutishia kumuua msichana wa miaka 14.

- Leo ninaomba kusimama hapa na kusema kwamba hii habari ni uongo na ni uzushi wa hali ya juu sana uliotengeenzwa na msichana mzoefu wa uzushi ambaye kwanza si kweli kwamba ni Mwanafunzi, pili ni Mtumzima mwenye mtoto tayari hata kabla hajakutana na Mh. Kapuya, pia ni muongo na mzushi mzoefu aliyewahi kuwadanganya pamoja na Mkurugenzi wa CRDB Bank, pamoja na kuidanganya TAMWA ambayo iliishia kumuripoti polisi na kuishia kwake kukaa rumande Segerea kwa muda mrefu sana.

- Kwa nini niliaiamini hii hadithi ni kwamba kuna siku mimi binafsi tulikuwa tumekaa faragha na Viongozi wengine Watatu wakubwa wa Taifa ambapo mbunge mmoja aliyedai kuijua kwa undani hii hadithi na kuhusiaka nayo, alianza kutuelezea hii hadithi kwa kutmia details kubwa kubwa sana, binafsi nilikuwa ninamuamini sana yule mbunge mpaka leo nilipothibitisha kwa 100% kwamba hii hadithi haiko sawa either na yeye ni muongo wa makusudi mwenye nia mbaya na Mh. Kapuya au na yeye alidanganywa na huyu msichana, ambaye jina lake kamili ni Hamida as opposed na majina mengi ya uongo ambayo amekuwa akiyatumia kudanganyia watu.

- Ninaomba kuwa wa kwanza kubeba huu msalaba, najua kwamba sio rahisi kueleweka na wengi ambao tulishamuhukumu Mh. Kapuya, lakini ukweli ni kwamba ni hadithi ya kutunga iliyoutngwa na msichana mmoja aliyebobea katika uzushi na uongo wa hali ya juu sana. Majuzi Waziri mmoja ninayemuamini sana katika Serikali ya sasa alinishitua kwamba hii hadithi ni ya uongo niiifuatilie tena, lakini sikuamuamini mpaka leo asubuhi sana nilipopigia sim na gazeti moja maarufu sana la Udaku, walioniambia kwamba hii habari si ya kweli na kwamba wanaye huyu msichana pale ofisini kwao, toka asubuhi mpaka sasa nimekuwa kwenye uhakiki wa hii ishu, na sasa ninasema wazi na tena kwamba:-

NINAMUOMBA RADHI SANA MH. KAPUYA NA NI MATUMAINI YANGU MAKUBWA SANA KWAMBA WALE WOTE TULIOHUSIKA NA KUMHUKUMU TUTAKUBALI MAPUNGUFU YETU KAMA WANADAMU NA KUMUUNGAMIA CHINI MUNGU WETU, NI KWELI MH. KAPUYA ALIKUWA NA MAHUSIANO YA KIMAPENZI NA HUYU BINTI LAKINI YA HIARI SIO KAMA ILIYOELEZWA NA SI KWELI KWAMBA HUYU BINTI NI MWANAFUNZI, HAPANA ANA MTOTO TAYARI NA PIA ALISHAWAHI KULIDANGANYA JESHI LA POLISI HUKO NYUMA.

- Wale wote tunahusika na media tujifunze tena na hili fundisho, tujitahidi kuwa waadilifu na kufanya utafiti wa kina kabla ya kuruka na hadithi nzito kama hii ambayo inaweza kummaliza mwananchi mwenzetu, au kiongozi bila sababu za msingi wala ukweli.


- AGAIN NI MATUMAINI YANGU KWAMBA WALE TULIOHUSIKA NA KUMHUKUMU MHESHIMIWA KAPUYA, TUTAJITOKEZA TENA IN THE PUBLIC NA KUMUOMBA RADHI NA MSAMAHA.

- MUNGU IBARIKI TANZANIA NA KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!


Le Mutuz The King Of All WASENGE Network Social MediaBlogu ya Wananchi.