KITENDA WILI"NYUMBA YANGU NDOGO LAKINI INAENEA WATU WENGI' MBUTA NANGA!!

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO BLOG

FLORA LYIMO BLOG

FLORA

FLORA

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA MH PINDA

FLORA NA MH PINDA

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

Monday 23 June 2014

WHATS ON ? JOYCE KIRIA ASEMA YOTE KUMHUSU MME WA FLORA MBASHA '' SHIKAMOO AKILI DADA JOYCE"

FRORA MBASHA POLE SANA...
NIJUAVYO MIMI NI KWAMBA, WAANDISHI WA HABARI NA VYOMBO VYA HABARI TUNAONGOZWA NA KANUNI NA SHERIA! NA KAZI KUBWA NI KUIELIMISHA JAMIIBADALA YA KUKANDAMIZA NA KUPOTOSHA JAMII. KWA
JINSI HIYO NI LAZIMA IFIKE MAHALI TUONE KWAMBA KUMDHALILISHA MTU ,PAMOJA NA KUINGILIA UHURU WA MTU BINAFSI NI MAKOSA!


Kinachoe delea sasa ivi juu ya Flora&Mbasa ni kwamba tunaingilia maisha binafsi ya mbasha na mbaya zaidi tunamdhalilisha ''MWANAMKE'' Flora..kwa sasa tunauza sana magazeti na tunapata trafiki kubwa kwenye blogs zetu ili kujiingizia kipato..kwa Kumdhalilisha Flora ndicho kinachoendelea...

Kama tumeamua kuchukua jukumu la Mahakama sawa. Maana ndicho tunachokifanya kila kona kujaribu kutoa hukumu ya kesi hii! Mbaya zaidi 99% tunamuhukumu Flora eti kwa misemo kwamba MWANAMKE MPUMBAVU hubomoa nyumba yake mwenyewe!

Ni lini huu mfumo dume ndani yetu utaondoka? Kosa linalomkabili mume wa Flora liko wazi wazi, na vitendo hivyo vinafanyika sana sana ndani ya nyumba zetu. Ni vitendo vya kumdhalilisha Mwanamke sana na vinatuumiza sana kina mama wengi. Hakuna mwanamke atakaependa kusikia mumewe kamdhalilisha kwa kulala na mwanamke mwingine. Tena mdogo wake??! Tena kwa kubaka! Hakunaaaaa! Hayupo huyo mwanamke...

Nikijaribu kuvaa viatu vya Flora ni vizito sana. Wala sijui ningefanya nini kwa maumivu ninayohisi....

Kinachoniumiza ni kwamba jamii imeacha HOJA ya msingi ambayo ni kitendo alichofanya Mbasha na ndicho kimempandisha kizimbani Mbasha!! na badala yake jamii kuanza kumuona Flora ni mkosefu kuliko aliyebaka..

Kwa maneno mengine ni kwamba tunabariki alichokifanya mbasha, na kwamba Mwanamke yeyote asichukue hatua yeyote endapo Mume atabaka au kutoka nje ya Ndoa yake.

Yaani mnatuambia wanawake wa nchi hii kwamba, ukimfumania mumeo au akibaka we umsamehe kimya kimya na maisha yaendelee! Mpaka sasa jamii haioni kwamba Mbasha amefanya kosa kabisa! Kana kwamba kama Mbasha hatakiwi kukemewa bali asifiwe mwanzo mwisho na zawadi apewe kwa kitendo hicho kama atakutwa na hatia kwamba amefanya...

yaan kwenye jamii yetu inaonekana mwanaume kua na mahusiano nje ya nyumba yake ni Sifa tena anapewa majina mazuri ya urijali! lakini kwa mwanamke ni umalaya na Ukahaba...

Hapo ndo napataga wazimu wa kichaga aiseee... Inaniumiza sana na kuna siku nilikaa nikaamua kuvunja ukimya juu ya hili jambo la michepuko tena nikawataja wazi wazi watu tunaowategemea wawe mifano bora lakini wao ndo waharibifu wakubwa! Cha ajabu jamii iliinuka juu yangu ila ukweli ulisimama na unabaki palepale kwamba mtu anapotoka nje ya Ndoa yake au nyumba yake ni MZINZI na anatakiwa akemewe bila kuangalia Hadhi yake.

kinachofanyika sasa kwenye jamii ni UNYANYASAJI DHIDI YA MWANAMKE NA UKATILI WA KIJINSIA pale tunapowaona wanaume WAzinzi ni marijali na Wanawake ndo Malaya na makahaba...

mbaya zaidi kuna baadhi ya wanawake wenzetu wanaushadadia huu MFUMO DUME kiasi kwamba wanakua mstari wa mbele kumnyooshea Flora vidole huku wakisahau kua mwenzio akinyolewa na ww zako tia maji..WANAWAKE TUSIMAME IMARA KUTOKOMEZA UKATILI NA MFUMO DUME kwenye jamii yetu...Kama kuna mwanamke atakaesherehekea mume wake akimbaka mdogo wake basi huyo amnyooshee kidole Flora...

Nasisitiza! ni kwa nn mwanaume husifiwa kwa uzinzi Na jamii inatetea???! HUU NI MFUMO DUME na ni Ukatili dhidi ya Wanawake...

MIMI JOYCE KIRIA NASEMA, MAADILI YAZINGATIWE NA WATU WOTE BILA KUJALI WADHIFA WA MTU. NA ENDAPO MTU AKIKENGEUKA BASI JAMII IMKEMEE VIKALI. BADALA YA KUTUKUZA UZINZI KWA KUANGALIA STATUS ZA WATU NA KUKANDAMIZA WANAWAKE....

kwa pamoja tunaweza kutokomeza ukatili huu.....

NOTE: WAKINA MAMA TUPIGE MAGOTI TUMLILIE MUNGU ASEME NA HAWA WATU WANAOTAWALIWA NA PEPO MCHAFU WA UZINZI..IN THE MIGHT NAME JESUS I PRAY...

FLORA LYIMO >SAY DADA JOYCE UMEYASEMA MANENO YANGU YOTE KUHUSU KESI HICHI '' SINA HATA MOJA LAKUONGEZEA'.
 

1 comment:

  1. wachagga na maendeleo ,shikamoo pesa flora lyimo ..mimi nakupenda sana kwa kazi zako ''asante kwa mzigo wangu nimeupata jana ''I LOVE IT''

    ReplyDelete