KITENDA WILI"NYUMBA YANGU NDOGO LAKINI INAENEA WATU WENGI' MBUTA NANGA!!

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO BLOG

FLORA LYIMO BLOG

FLORA

FLORA

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA MH PINDA

FLORA NA MH PINDA

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

Saturday 2 March 2013

HUYU NDO YULE MTOTO ALOPOTEA JANA MCHANA TUKAWA TUNAMTAFUTA YANI NILIACHA SHUGHULI ZANGU NA KUANZA KUMFARIJI MAMA YAKE HADI POLICE WAKAJA !!

Hapa akiletwa na Police ndo anapelekwa kwa Mama yake kipenzi aliyekuwa anahuzuni analia kama Mtoto mdogo" kweli leo nimejua Uchungu wa mwana aujuae ni MAMA" kwani Mtoto huyu yeye anacheka na nikama hata hajafanya kosa lolote,,Yesu na Maria,angekuwa ni Kule Bongo angechapwaje leo" Uwiii"
 Here he is" His name is Blessing" and for sure ni Blessing wa ukweli ,kama anaweza kujiondokea zake mtoto only 4years old hajui anakoenda bali anachokifanya na hizo akili zake za miaka minne na kukutwa salama ni Mungu anajua"kwani tushawahi kuona Makubwa ya watotokupotea na mwisho kuonekana wakiwa wafu au kutokuonekana kabisa" I feel for her mum so much !!
 Hapa akutanishwa na Mama yake ndani ya lile lile duka la vipodozi na nywele in Dalston " yani alikuwa anafuraha ni kama hata hajamtia Mama yake Wasiwasi mkubwa na kulia kama Mtoto! Yani hii picha na hiyo ya hapo juu nilipiga na sim yangu kwani akili za kuniambia nipige na Camera zilikuwa hata hazijanijia kwani was so so happy Blessing kapatikana Mzima na Mikonono mwa Mama yake kipenzi"
 Then hapa akili zimenijia nikaanza kupiga picha na Camera yangu ila walikuwa na haraka yakuendelea ku fanya shopping zao na mimi nikawaondokea na kuendelea na shughuli zangu !!
 Yani huyu mtoto anaonekani ni mwerevu na hodari ,si mchezo muone hapa pichani ni baada yakupotea na kurudishwa kwa Mama yake na huku angalia huyu alomshikilia mkono ni mama yake na bado hata hajisikii yeye anajisikia kuburutana na Dada yake,ambae pia wapo pamoja na wakati wakuwatoroka walikuwepo wote watoto watatu na Mama yao, Dada yake ni kashichana kadogo kama miaka tisa na kachanga chao pengine mwaka mmoja"
Hapa nimewapiga picha kwa nyuma wakiendelea na shughuli zao za kufanya shopping " mnaliona hilo basi mbele hapo ndo 149 linalokwenda Edmonton Green ambalo huyo mtoto ndo kama hilo alipanda mwenyewe baada ya kuwatorekea Familia yake wakiwa Dukani ,basi Mama kaanza kutafuta mtoto peke yake anapanda na kushuka kwa masaa mawili hadi kasema karudi nyumbani kwenda kuangalia ikiwa kaenda nyumbani peke yake lakini wapi,,sasa aliporudi Dukani pale kwa mara nyingine ndo wakaamua waite Police,,sasa mimi nikamgombeza na kumuambia kwanini hujaita Police mara moja" wakati ukiwa hapahapa Dukani hujaondoka ulipomkosa mwanao ?akakosa lakusema nikamuambia mbele za mapolisi walokuwepo ,,next time please call the Police mara hiyo hiyo Police wapo kwa Mambo kama haya ndiyo maana wapo na pia wanauwezo wakuangalia cameras na pia hata wapita njia,jua wapo  kwa ajili ya vitu kama hivi'haswaa" Basi hata Police wakawa wamekubaliana na mimi na kumuambia hata ikiwa ni kitu chochote kimefanyika nyumbani au popote na hujui lakufanya ita Police watakuambia ikiwa wanahitajika au la" yani nilikuwa na huzunika alafu nawaza vile ile habari mbaya mno ya watoto walishawahi kumshika mtoto mwenzao na kumuiba shopping centre akiwa na mama yake hivi hivi na wakaenda kumuuwa mtoto yule..yani nilikuwa nasali sana kimoyo moyo" and thanks God Police wakapigiwa sim pia wakaambiwa kuna mtoto kapotea amepatikana Edmonton Green " na kumbe ni haka katoto kalienda na basi mpaka mwisho wa basi ndipo Dereva wa basi kamstukia yupo kwenye basi kabakia huko peke yake,ndo kumuitia Police!! HABARI NDO HIYO MTOTO SASA YUPO NA FAMILIA YAKE HASA MAMA YAKE NA DADA YAKE AMBAO WALIKUWA NA HUZUNI KUBWA KUMPOTEZA KIJANA WAO ONLY 4 YEARS OLD"  GOD IS GREAT" Ila Wazazi kuweni waangalifu sana na watoto wenu washikilieni mikono kila wakati hasa njiani mnapotoka nao kwani kuna mpaka na watu wanaoiba watoto so mara hii imekuwa kajiendea mitoko yake mwenyewe lakini mara nyingine hutaki kusikia kaibwa na vile vijidudu watu vyakuwaiba watoto na kuwafanyia makuu na mwisho wa siku kuwauwa!!

No comments:

Post a Comment